Main Menu

Monday, April 15, 2013

NICOLAS MADURO AMRITHI HUGO CHAVEZ BAADA YA KUCHAGULIWA KATIKA UCHAGUZI WA JANA WA RAIS NCHINI VENEZUEL

Katika uchaguzi wa urais nchini Venezuela, Nicolas Maduro, mrithi wa aliyekuwa rais wa taifa hilo, Hugo Chevez, ameshinda kwa kupata asilimia 51 ya kura. 

Huo ulikuwa uchaguzi wa kwanza kufanyika nchini humo tokea kufariki kwa kiongozi wa kisoshalisti, Hugo Chavez. 

Hata hivyo mshindani wake, kiongozi wa upinzani Henrique Capriles, ambaye pia ni Gavana wa jimbo la Miranda, alijijenga katika umaarufu mnamo siku za karibu hadi kufikia asilimia 7 nyuma ya Maduro. 

Kiongozi huyo wa upinzani, Henriuqe, aliyeshindwa  na hayati Chavez katika uchaguzi wa mwaka jana, amelalamika juu ya uchaguzi huo. 

Amemlaumu Rais wa sasa Maduro kwa kuyatumia vibaya mamlaka ya serikali na kwa kukiuka sheria za uchaguzi. 

Kwa upande wake Maduro alidai kwamba kambi  ya mrengo wa kulia iliendesha kampeni chafu dhidi yake.

0 comments:

Post a Comment