Main Menu

Monday, June 1, 2015

BUSUNGU ATAMBULISHWA RASMI YANGA, AKABIDHIWA JEZI YA NIZAH KHALFAN



Mshambuliaji mpya wa klabu ya Young African Malimi Busungu ametambulishwa rasmi leo makao makuu ya klabu hiyo.

Katika utambulisho wake Busungu amekabidhiwa jezi namba 16 iliyokua inatumiwa na kiungo Nizah Khalfan anayedaiwa kutimukia timu ya Mwadui Fc.

Katika utambulisho huo busungu amesema kucheza Young African ni sehemu ya kukamilika kwa ndoto yake na zaidi ni kuwa timu hiyo inashiriki michuano ya kimataifa.
 
Amesema kama ilivyo kwa mchezaji mwingine yoyote ni vigumu kukataa kuchezea timu kama Young African.
Busungu alisain kuichezea Young Afriican kwa mkataba wa miaka 2 siku ya jumamosi akitokea timu ya Mgambo JKT aliyoichezea kwa mafanikio.

Kwa upande wa mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano wa klabu hiyo Jerry Murro amesema hivi sasa wamefunga usajili wa wachezaji wa nyumbani na sasa wanaanza usajili wa kimataifa na ikiwezekana wiki ijayo watamtambulisha moja ya wachezaji bora kabisa afrika.
 
Kuhusu idadi ya wachezaji ambao wataachwa na timu hiyo msimu huu, Jerry alikua mgumu kuwataja kwa majina lakini akasisitiza wachezaji hao tayari wanazo taarifa za kutoendelea kuwa na timu hiyo, na kiashiria cha kutokua nao ni namba ya jezi walizokua wanavaa kupewa wachezaji wengine.

0 comments:

Post a Comment