Main Menu

Monday, June 1, 2015

MBEYA CITY YAKAMILISHA USAJILI WA GIDION BROWN WA NDANDA FC



Timu ya Mbeya City imeendelea kuboresha kikosi chake baada ya kumsajili mshambuliaji wa timu ya ndanda fc gidion brown.

Kwa mujibu wa website ya timu hiyo Mshambuliaji huyo ameingia mkataba wa mwaka mmoja na nusu kuwatumikia wagonga nyundo hao wa jiji la mbeya.

Msimu uliopita Brown alikuwa moja ya wachezaji muhimu kwenye kikosi cha Ndanda Fc akicheza michezo  21 akiwa kwenye kikosi cha kwanza, na kuifungia timu hiyo ya Mtwara jumla ya mabao 5.
 
Awali mshambuliaji  huyu amewahi kuchezea timu ya KMKM ya  Zanzibar na kuisaidia kutwaa taji la ligi kuu ya visiwani humo pia amecheza kwenye kikosi cha Rhino ya Tabora na Moro United.

0 comments:

Post a Comment