Main Menu

Friday, May 29, 2015

OFA YA LIVERPOOL KWA SOUTHAMPTON YAKATALIWA



Liverpool will increase their offer for Nathaniel Clyne at Southampton after an initial bid was rejectedOfa ya Klabu ya Liverpool ya paun milioni 10 kwaajili ya kutaka kumsajili mlinzi wa kimataifa wa  England Nathaniel Clyne imekataliwa na Southampton. 

Lengo la Liverpool kutaka kumsajili Clyne, mwenye umri wa miaka 24,  ni kutaka kuziba pengo la Glen Johnson, mwenye umri wa miaka 30, ambaye mkataba wake unamalizika. 

Clyne alijiunga na watakatifu hao akitokea Palace mwezi July mwaka 2012  mkataba wake unamalizika mwaka 2016. 

Aidha Liverpool pia inatajwa kutaka kumsajili mshambuliaji wa Burnley Danny Ings pamoja na kiungo wa Manchester City James Milner. 

Msimu uliopita Liverpool iliigeuza Southampton gulio  kwa kuwasajili Adam Lallana, Dejan Lovren na Rickie Lambert wote watatu kwa paun milion 50.

0 comments:

Post a Comment