Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania (Taifa
Stars) kimewasili salama jana Mjini Johannesburg kwa ajili ya maandalizi ya
mwisho kabla ya kwenda Maputo, Msumbiji kwa ajili ya mechi dhidi ya Mambas
itakayochezwa Jumapili.
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro
Premium Lager imefanya mazoezi mara mbili leo asubuhi na jioni kwenye uwanja wa
Bed ford view Country Club.
Mazoezi ya mwisho yatafanyika kesho
asubuhi kabla ya jioni kuanza safari kuelekea Maputo.
Wakati huo huo, Balozi wa Tanzania nchini
Afrika Kusini, Razia Msuya leo jioni amezitembelea timu zote mbili za Tanzania
zilizopo Johannesburg kusalimia wachezaji.
Serengeti Boys yenyewe ipo Mjini humo
tangu Julai 27 kwa ajili ya mechi dhidi ya Afrika Kusini itakayochezwa Agosti 2
mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment