Mshambuliaji
wa Taifa Stars, Mbwana Samatta amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwaka
na mashabiki wa klabu yake ya TP Mazembe katika ya mchezaji bora wa
mwaka wa klabu hiyo iliyopewa jina la “Corbeau d’Or”. Samatta ambaye
amepewa jina la utani la “Samagoal” na mashabiki wa TP Mazembe
aliwabwaga wachezaji wengine watano waliokuwa wakishindana.
Baada ya zoezi zima la upigaji kura matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:
1. Mbwana Samatta – Kura 248
2. Asante Solomon – Kura 219
3. Robert Kidiaba – Kura 200
4. Nathan Sinkala – Kura 97
5. Rainford Kadaba – Kura 67.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment