Main Menu

Wednesday, August 14, 2013

REDDS MISS ILALA TALENT KUFANYIKA LEO


KATIKA Kuelekea Redds Miss Ilala Ijumaa, leo kutakuwa na shindano la kumtafuta mrembo mwenye kipaji (Talent) itakayofanyika katika mgahawa wa City Sports and Lounge uliopo katikati ya jiji.
Mratibu  wa shindano hilo, Juma Mabakila  alisema kuwa maandalizi ya kuelekea shindano hilo yanaendelea vizuri na kueleza kuwa warembo wote 14 wamejipanga kuonesha vipaji vyao ipasavyo.
Mabakila alisema mshindi wa talent atakabidhiwa zawadi zake kwenye fainali ya shindano hilo ambalo litafanyika Ijumaa ijayo  katika ukumbi wa Golden Jubilee Tower ulipo katikati ya jiji.
Mratibu huyo wa Ilala alisema mbali ya burudani hiyo, pia watatumia nafasi hiyo kuuza ticket za VIP ambazo ni chache kwa watu maalum, lakini kutakuwa na bahati nasibu itakayotoa pasi za bure za kusingia katika onesho la Ijumaa.
Alisema kwamba shindano la mwaka huu litaandika historia mpya ya urembo kwa wilaya ya Ilala maana wamejipanga na kupata sapoti ya kutosha, hivyo mashabiki wa mashindano ya urembo wakae mkao wa kupata raha.
“Tumejipanga vizuri kuonesha shoo nzuri kuanzia hii ya telent na ile kubwa Ijumaa, kutakuwa na vitu tofauti na ilivyokuwa mwaka jana, kweli mambo yanakwenda vizuri,” alisema  Mabakila.
Mashindano ya Redd's Miss Ilala yamedhaminiwa na Redd's Original,magazeti ya Jambo Leo, Tanzania Daima,Smile, CXC Safaris, Blog ya wananchi, Fredito na Dodoma wine

0 comments:

Post a Comment