Main Menu

Monday, July 1, 2013

MAADHIMISHO YA SERIKALI ZA MITAA MKOANI IRINGA, WANANCHI WATAKIWA KUTOZIOGOPA OFISI ZA MANISPAA KUHOJI MASUALA MBALIMBALI

 maandamano yakielekea katika uwanja wa mwembetogwa.
 Maandamano yakiingia uwanjani mwembetogwa

  Mkuu wa wilaya ya Iringa Dr Letisia wWrioba akikagua mabanda mbalimbali katika uwanja huo



 Mkuu wa wilaya Dr Warioba akizima moto baada ya kutembelea gari la zima moto
 Mchungaji Peter Msigwa akizungumza na wananchi na wakuu wa idara za manispaa ya Iringa




Wakati maadhimisho ya serikali za mitaa yakifanyika leo, Wananchi wametakiwa  kutoziogopa ofisi za manispaa kwa ajili ya kuhoji masuala ya maendeleo, sanjari na kusoma rasimu ya katiba mpya na kutoa maoni .


Akiwahutubia wananchi na watumishi wa idara mbalimbali za manispaa ya Iringa, Mgeni rasmi katika maadhimisho ya serikali za Mitaa, mkuu wa wilaya ya Iringa Dr Letisia Warioba mbali ya kuwaagiza waandaaji wa maadhimisho hayo kuwaalika viongozi wa ngazi za chini katika maadhimisho yajayo,  ametoa wito kwa wananchi kutoa maoni ya katiba mpya kupitia mabaraza ya katiba.


Akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za halmashauri ya Manispaa ya Iringa kaimu mkurugenzi Imaculeti Senje, amesema ugonjwa wa malaria umeendelea kuongoza kwa vifo manispaa ya Iringa.



Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa amewataka wananchi wa manispaa hiyo kutoziogopa ofisi za manispaa na badala yake wajitokeze kuhoji na kupata ufafanuzi wa mambo mbalimbali yanayowakabili.


Maanzimisho hayo kwa manispaa ya iringa yamefanyika katika viwanja vya mwembetogwa wakati ya kitaifa yamefanyika mkoani morogoro wakiwa na kauli mbiu isemayo  ‘AMAN, UADILIFU KWA WOTE NI NYENZO MUHIMU KATIKA MCHAKATO WA KATIBA MPYA NA USTAWI WA SERIKALI ZA MITAA’.

0 comments:

Post a Comment