1. Mwaka 1926 J.L BAIRD alitengeneza TV ya
kwanza ambayo uwezo wake wa kuonyesha ulikua wa kiwango cha mistari 30 tofauti
na TV za sasa zenye mistari mpaka 1080 ambayo ni high definition.
2.TV
ya Panasonic ya Inch 150 ndio TV kubwa kuliko zote kwa sasa ambayo gharama yake
ni dola laki moja za Kimarekani sasa hivi, pesa ambayo kibongobongo ni zaidi ya
milioni 150.
3.Tangazo la kwanza kwenye TV liliruka
hewani kwa mara ya kwanza siku ya kwanza ya July mwaka 1941 na lilihusu mechi
ya mpira wa Baseball Marekani kati ya B. DODGERS NA PHILADELPHIA PHILLIES na
lilikua la sekunde 20, gharama yake wakati huo ilikua dola 9 za Kimarekani
ambayo kwa bongo ni zaidi ya shilingi elfu 10.
4.Kwa Marekani, watoto mpaka kufikia
umri wa miaka 14 wanakua wameshuhudia matukio elfu kumi na moja ya mauaji
kupitia TV.
5. Kipindi cha miaka ya 1950
kilifahamika kama zama za dhahabu kwa Televisheni, ni wakati ambapo matangazo
ya kwanza ya rangi yaliruka, kabla ya hapo yalikua yanaruka ambayo ni black and
white.
6.Remote ambazo hutumika kubadilishia
channel na vitu vingine kwenye TV zilianza kutumika kwenye miaka ya 1980.
7. Matukio yaliyoweka rekodi ya
kutazamwa sana kwenye TV ni michezo ya Olympic na michuano ya FIFA ya kombe la
dunia.

0 comments:
Post a Comment