Main Menu

Wednesday, July 24, 2013

JE UMEANZA KUTUMIA TV LINI? UNAFAHAMU ZILIPOTOKA? NA TV KUBWA KABISA INAUZWAJE?

 
1. Mwaka 1926 J.L BAIRD alitengeneza TV ya kwanza ambayo uwezo wake wa kuonyesha ulikua wa kiwango cha mistari 30 tofauti na TV za sasa zenye mistari mpaka 1080 ambayo ni high definition.

2.TV ya Panasonic ya Inch 150 ndio TV kubwa kuliko zote kwa sasa ambayo gharama yake ni dola laki moja za Kimarekani sasa hivi, pesa ambayo kibongobongo ni zaidi ya milioni 150.


3.Tangazo la kwanza kwenye TV liliruka hewani kwa mara ya kwanza siku ya kwanza ya July mwaka 1941 na lilihusu mechi ya mpira wa Baseball Marekani kati ya B. DODGERS NA PHILADELPHIA PHILLIES na lilikua la sekunde 20, gharama yake wakati huo ilikua dola 9 za Kimarekani ambayo kwa bongo ni zaidi ya shilingi elfu 10.

4.Kwa Marekani, watoto mpaka kufikia umri wa miaka 14 wanakua wameshuhudia matukio elfu kumi na moja ya mauaji kupitia TV. 

 5. Kipindi cha miaka ya 1950 kilifahamika kama zama za dhahabu kwa Televisheni, ni wakati ambapo matangazo ya kwanza ya rangi yaliruka, kabla ya hapo yalikua yanaruka ambayo ni black and white.

6.Remote ambazo hutumika kubadilishia channel na vitu vingine kwenye TV zilianza kutumika kwenye miaka ya 1980.

7. Matukio yaliyoweka rekodi ya kutazamwa sana kwenye TV ni michezo ya Olympic na michuano ya FIFA ya kombe la dunia.

8. Mwishoni mwa vita kuu ya pili ya dunia, Televisheni iligeuka kuwa rahisi kwenye umiliki kwa yeyote anaeweza kumudu gharama za kuinunua.
 

0 comments:

Post a Comment