Main Menu

Thursday, June 20, 2013

WANANCHI MKOANI IRINGA WAINGIA MITAANI KUWASAKA VIBAKA WANAOSADIKIKA KUWAPIGA WATU NONDO NYAKATI ZA USIKU

    Mtuhumiwa huyo akipelekwa huku akipatiwa kipigo cha maana
                      Kibaka akiendelea kupata kichapo............
Wananchi nje ya kituo cha polisi mkoa wa iringa karibu na soko kuu
Mmoja wa vijana akionyesha mkono ukiwa umechafuka damu kutokana na kutoa kipigo kwa kibaka huyo
                                   kamata kamata mwizi mitaani
     wananchi mitaani wakiwa na dhana zao za jadi
        Hapa ilikua kwenye kilabu kimoja cha pombe za kienyeji wakimtafuta kibaka mwngine
Wananchi wakimpeleka mmoja wa vibaka hao kituo cha polisi huku polisi wakijitahidi kumuwekea ulinzi asiendelee kupigwa



Wananchi mkoani iringa hii leo wemeingia mitaani kuwatafuta, kuwapiga, na kuwakamata na kuwapeleka polisi vibaka wanaodaiwa kuwa wapiga nondo nyakati za usiku.

Hatua hiyo imekuja baada ya kijana mmoja anayefahamika kwa jina la salmu kuvamiwa na kuporwa na vibaka hao siku ya jumamosi ambapo aliporwa simu pamoja na fedha akiwa na wenzake wawili.

Baada ya kijana huyo kupona majeraha aliyoyapata alifanikiwa kumpata mmoja wa kijana aliyempora kwa kuwa alimkariri usiku ule na kuwajulisha vijana wenzake ndipo walipomvamia na kumpa kichapo cha maana na kuwataja wenzake walioshirikiana nae usiku ule.

Kundi hilo la wananchi lilifanikiwa kuwakamata vijana watatu huku msako ukiendelea kwa kijana mwingine ili kukamilisha list ya waliotajwa.
Hatua hiyo imekuja baada ya kukithiri kwa vitendo vya upigaji nondo klatika maeneo ya  manispaa ya iringa zaidi kata za kitanzini na mivinjeni.

0 comments:

Post a Comment