Main Menu

Wednesday, March 13, 2013

WAANDISHI WA HABARI WA KIGENI WASIO NA VIBALI KUSHTAKIWA KENYA



Serikali ya Kenya ilionya hapo siku ya Jumatano (tarehe 13 Machi) kwamba waandishi wote wa habari wa kigeni nchini humo wasio na vibali maalum kutoka Wizara ya Habari na Mawasiliano watashtakiwa.


"Tuna waandishi wengi wa kigeni nchini mwetu na hatujuwi wanafanya kazi vipi," alisema Mkurugenzi wa Mawasiliano Joseph Owiti, kwa mujibu wa kituo cha Capital FM cha Kenya.

 "Tunaweza kuhitaji msaada wa maafisa wa usalama kuwatambua watu hao waliopo hapa kinyume na sheria."


Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Umma, Mary Ombara, alisema serikali imekuwa na wasiwasi na "kazi mbaya inayofanywa na baadhi wa waandishi wa kimataifa katika kuuripoti uchaguzi."


"Katika hili, tunafurahi kwamba vyombo vya habari vya hapa vilikataa kuchukua habari za uongo juu ya kununuliwa kwa maelfu ya mapanga au picha iliyorushwa kuonesha ghasia ambazo hazipo nchini," alisema.

 "Habari lazima kila siku ziwe za ukweli na zisizopendelea upande wowote."


Mkuu wa Idara ya Leseni za Filamu, Ernest Kerich, alisema waandishi wengi wa kigeni walioruhusiwa kuripoti uchaguzi mkuu bado wapo nchini bila ya vibali muafaka.


"Tumejulishwa kwamba baadhi ya waandishi wa habari waliendelea kubakia na kujihusisha na kutengeneza filamu fupi wakitumia vibali vile vile walivyopewa," alisema Kerich. 

"Hilo sio tu linavunja sheria za nchi, bali pia linaikosesha nchi mapato."

0 comments:

Post a Comment