Main Menu

Thursday, March 14, 2013

SIKU CHACHE BAADA YA KUINGIA MADARAKANI UHURU KENYATTA KUPUNGUZA MISHAHARA

Uhuru kenyatta rais wa nne wa kenya

Rais-mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto wameonya kuwa Kenya haiwezi kumudu gharama za mishahara na hivyo wamesema serikali yamkini ikakata mishahara hiyo au kusimamisha nyongeza ya mishahara.

Wawili hao wakizungumza Jumatano wamesema huenda Kenya ikapoteza nafasi yake ya kiuchumi barani Afrika kutokana na bajeti kubwa ya mishahara. 

Uhuru amesema serikali yake itajitahidi kupunguza bei za bidhaa muhimu ili wakati mishahara itakapopunguzwa, Wakenya wawe na uwezo wa kujidhaminia maisha bora.

Kwa upande wake makamu wa rais mteule William Ruto amesema Kenya inatumia asilimia 12 ya Pato Ghafi la Ndani au GDP kugharamia mishahara ya watumishi wa umma katika hali ambayo nchi zingine za Afrika kusini mwa jangwa la Sahara hutumia chini ya asilimia saba ya GDP kulipia mishahara ya watumishi wa umma.

Amesema hicho ndicho kiwango wastani duniani ambacho huwezesha kuwepo ustawi endelevu. 

Matamshi hayo yanakuja siku moja baada ya Tume Inayoshughulikia Mishahara ya Maafisa wa Umma Kenya kupunguza mishahara ya wabunge kwa asilimia 37 kutoka shilingi 850,000 hadi 532,500. 

Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2011, serikali ya Kenya ina wafanyakazi takribani 220,000.

0 comments:

Post a Comment