Main Menu

Monday, February 23, 2015

HIVI NDIVYO YANGA WALIVYOWAUA WANYAKYUSA UWANJA WA SOKOINE



Timu ya yanga jana imeongeza pengo la point dhidi ya mpinzani wake Azam fc baada ya kupata ushindi wa mabao matatu kwa moja mbele ya Mbeya City.

Yanga sasa imefikisha alama 31 nne juu ya azam waliopo nafasi ya pili baada ya jana usiku kulazimishwa sare ya bila kufungana na timu ya Prison kutoka mbeya mchezo uliofanyika katika uwanja wa azam Complex Dar  es salaam.

Katika mchezo wa jana wa Yanga timu hiyo iliruhusu goli katika lango lake baada ya kuchezo michezo saba bila kuruhusu goli.

Magoli ya yanga ya jana yalifungwa na Simon Msuva
katika dakika ya 18 alipounganisha kwa kichwa krosi ya Oscar Joshua, magoli mengine yalifungwa na Mrisho Ngassa na Amisi Tambwe.

 Simon Msuva akishangilia bao lake la kwanza mbele ya timu ya Mbeya City
 Tunawaua
 kocha wa yanga Hans Van Pluijm akiteta na vijana wake
 Ngassa akifanya yake sokoine
 Mwenyekiti wa CHADEMA Freman Mbowe akiwasili uwanja wa Sokoine na mwenyeji wake mbunge wa jimbo la Mbeya mjini Joseph Mbilinyi SUGU.

 Ngassa akifunga bao la tatu la yanga


0 comments:

Post a Comment