NYOTA Cristiano Ronaldo amerejea
Manchester na kuifungia bao la ushindi Real Madrid lililoitoa timu yake
ya zamani katika Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu Uwanja wa Old
Trafford.
Sir Alex Ferguson alimuanzishia benchi
Wayne Rooney, lakini wenyeji ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao mapema
kipindi cha pili, baada ya Sergio Ramos kujifunga.
Lakini mambo yaliwaharibikia baadaye
kidogo tu Man United, baada ya Luis Nani kuonyeshwa kadi nyekundu ya
moja kwa moja kwa kumchezea rafu Alvaro Arbeloa.
Na baada ya hapo, bao la Luka Modric
lilifuatiwa na bao la Ronaldo dakika tatu baadaye, hivyo vigogo hao wa
Hispania kutinga Robo Fainali.

hapa ronaldo sijui alikua anawaomba msamaha mashabiki wa man u

Kiungo wa zamani wa Spurs, Modric akifunga bao la kusawazisha


ronaldo akiwaua ndg zake


Beki wa Real akijifunga


Kadi nyekundu: Hapa ndipo ilipofia United baada ya kupungukiwa mchezaji mmoja



Akitokea benchi: Rooney akipasha kutokea benchi


Welbeck alikaribia kufunga leo, lakini alikuwa ameotea


Vidic alipiga kichwa kikagonga mwamba kipindi cha kwanza


Giggs amecheza mechi ya 1,000 leo Man United


Ronaldo amepata mapokezi mazuri leo Old Trafford

Ronaldo alikuwa katika wakati mzuri leoOld Trafford

Ronaldo akipasua Old Trafford

0 comments:
Post a Comment