Main Menu

Sunday, January 13, 2013

MAKOMANDOO WA UFARANSA WAFELI SOMALIA

 
Rais  Francois Hollande wa Ufaransa amekiri kuwa makomando wa nchi yake wamepata pigo wakati wakijaribu kumkomboa jasusi Mfaransa anayeshikiliwa mateka na wanamgambo nchini Somalia.

Katika taarifa Jumamosi jioni, Hollande amesema makomando wawili wa kikosi maalumu cha Ufaransa waliuawa wakijaribu kumkomboa mateka ambaye pia aliuawa katika oparesheni hiyo.

Wakati huo huo wanamgambo wa Al Shabab wanasema kuwa bado wanamshikilia mateka huyo Mfaransa Denis Allex. Aidha wanamgambo hao wamedai kuwa wamemchukua mateka mwanajeshi wa Ufaransa.

Oparesheni hiyo iliyofeli ya Jeshi la Ufaransa ilitekelezwa Jumamosi alfajiri katika eneo la Buula-Marere yapata kilomita 110 kusini mwa mji mkuu wa Somalia Mogadishu. 

Walioshuhudia wanasema raia watano waliuawa katika mapigano makali kati ya makomando wa Ufaransa na wapiganaji wa Al-Shabab.  

Allex alitekwa nyara na wapiganaji wa Al-Shabab Julai 2009  akiwa katika shughuli za ujasusi nchini Somalia.

CHANZO RADIO TEHRAN

0 comments:

Post a Comment