Mamlaka ya Kodi na
Mapato nchini (TRA) inatarajiwa kuendesha semina ya kodi kwa viongozi wa vilabu
viliyopo jijini Dar es salaam, siku ya ijumaa tarehe 14 Agosti katika hoteli ya
Tiffany iliyopo eneo la Kisutu.
TRA itaendesha semina hiyo kwa vilabu vilivyopo ligi kuu,
ligi daraja la kwanza na ligi daraja la pili ambapo viongozi wakuu wa vilabu
hivyo, Katibu Mkuu, Mwenyekiti, na Mhasibu wanapaswa kuhudhuria semina hiyo.
Kwa kuanzia TRA itaendesha semina hiyo jijini Dar es
salaa, na baadae kuendelea na semina hizo kwa vilabu vilivyopo mikoani kwa
lengo la viongozi wa vilabu kutambua umuhimu wa ulipaji kodi kwa wachezaji, makocha
wanaowaajiri katika vilabu vyao.
Semina hiyo itaanza saa 3 asubuhi mpaka saa 5 kamili
asubuhi katika hoteli ya Tiffany iliyopo eneo la Kisutu jijini Dar es salaam,
vionggozi wa vilabu vya ligi kuu, ligi daraja la kwanza, ligi daraja la pili
waliopo jijini Dar es salaam mnaombwa kuhudhuria semina hiyo.
0 comments:
Post a Comment