Main Menu

Wednesday, July 8, 2015

WASHIRIKI SPORTS XTRA NDONDO CUP WAKABIDHIWA VIFAA




Timu zinazoshiriki michuano ya Sports Xtra Ndondo Cup hatua ya makundi zimekabidhiwa vifaa tayari kwa ajili ya hatua hiyo inayotarajiwa kuzinduliwa siku ya ijumaa.

vifaa hivyo vimekabidhiwa leo kwa viongozi wa timu hizo mbele ya mdhamini wa mashindano hayo Dr. Juma Mwaka wa kituo cha Foreplan Clinic.
 
Waratibu wa mashindano hayo Clouds Media Group kupitia kwa mkuu wa kitengo cha michezo Shaffih Dauda, amesema lengo la kuanzisha mashindano hayo ni kuwapa vijana nafasi ya kuonesha vipaji vyao na kujiepusha na vitendo vya kihuni.

Kwa upande wake mdhamin wa michuano hiyo Dr Juma Mwaka amesema uamuzi wake wa kudhamini mashindano hayo ni kutokana na michezo hivi sasa kuwa ajira.

Mashindano hayo hatua ya makundi yatazinduliwa siku ya ijumaa katika uwanja wa Bandari Tandika kati ya mabingwa watetezi Abajalo fc ya Sinza dhidi ya Kauzu Fc ya Tandika sokoni.
 
Kama ilivyo mwaka jana bingwa atajinyakulia kitita cha shilingi million tano, mshindi wa pili million 3, na mshindi wa tatu million 2, huku kikundi bora cha ushangiliaji kikiondoka na milioni moja.

0 comments:

Post a Comment