Main Menu

Sunday, May 31, 2015

BARCELONA KUTWAA COPA DEL REY KUMEONGEZA UTAMU WA FAINAL YA LIGI YA MABINGWA ULAYA JUNE 6

Barcelona stars pose on the pitch as they close in on a treble with only the Champions League final to playUsiku wa jana timu ya Barcelona imetwaa taji la pili msimu huu, baada kuifunga Athletic Bilbao mabao 3-1 katika fainali ya Kombe la Mfalme, maarufu kama Copa del Rey iliyofanyika katika Uwanja wa Nou Camp.
Lionel Messi aliendelea kuwa mtu hatari kwa wapinzani wake baada ya kufunga mara mbili huku akionesha uwezo wa hali ya juu pale alipowapangua mabeki wanne wa bilbao na kuifungia Barcelona bao zuri la kwanza dakika ya 20, kabla ya Mbrazil Neymar kufunga la pili dakika ya 36.The Argentina phenomenon beat four Bilbao defenders to score his 57th goal of another incredible season
Messi akakamilisha ushindi wa Barca kwa kufunga bao la 3 dakika ya 74, wakati bao la kufutia machozi la Bilbao lilifungwa na Williams dakika ya 79.
Barca sasa imechukua mataji mawili kwani awali ilishachukua kombe la La liga sawa na wapinzani wao wa ligi ya mabingwa katika fainal timu ya Juventus ya italia ambao tayari nao wana makombe mawili ya seria A na Copa Italia.
Hivyo kila timu inahitaji ubingwa wa UEFA ili kutwaa makombe matatu.Barcelona players link arms to celebrate on the pitch after claiming the King's Cup at the Nou Camp

0 comments:

Post a Comment