Main Menu

Friday, August 15, 2014

MWAMEJA KUWAONGOZWA WAKONGWE WA TANZANIA KUWAUA WAKONGWE WA REAL MADRID YA HISPANIA

Golikipa Mwameja Mohamed atakiongoza kikosi cha Tanzania All Stars kilichopewa jina la TSN Tanzania eleven kitakachomenyana na magwiji wa Real Madrid ya Hispania, Agosti 23, mwaka huu. 

Chini ya makocha Charles Boniface Mkwasa na msaidizi wake Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, Daktari Mwanandi Mkwankemwa na viongozi Mtemi Ramadhani, Hassan Mnyenye, Omar Gumbo na Hamisi Kisiwa kikosi hicho kitaingia kambini jumatatu ya tarehe 18 uwanja wa karume. 


Wengine walioItwa ni mabeki Nsajigwa Shadrack, Mecky Mexime, Boniface Pawasa, John Mwansasu,  Abubakar Kombo, George Masatu, Habib Kondo, 
Viungo Suleiman Matola, Shaaban Ramadhani, Salvatory Edward, Sabri Ramadhani ‘China’, Yussuf Macho, Abdul Mashine, Abdul Maneno, Mao Mkami, Steven Nyenge, Madaraka Suleiman, Akida Makunda na Mtwa Kihwelo.

Washambuliaji ni Monja Liseki, Iddi Moshi, Dua Said, Emmanuel Gabriel, Said Maulid, Thomas Kipese, Nasor Mwinyi ‘Bwanga’, Edibilly Lunyamila, Mohamed Hussein ‘Mmachinga’, Clement Kahbuka,  Madaraka Suleiman na Akida Makunda. 

Wachezaji waliotamba kuanzia La Liga, wakacheza ligi nyingine za Ulaya, Kombe la Ulaya, Ligi ya Mabingwa na Kombe la Dunia waliowahi kuchezea Real Madrid wanatarajia kuwasili nchini Agosti 22.

0 comments:

Post a Comment