Main Menu

Monday, December 16, 2013

LIPUMBA; KATIBA MPYA 2014 KWA TANZANIA HAIWEZEKANI

Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) nchini Tanzania, Profesa Ibrahim Lipumba amesema  kuwa, mchakato wa Katiba Mpya nchini humo una vikwazo vingi na kwamba Katiba haiwezi kupatikana mwaka 2014 kama Rais Kikwete alivyoahidi, hivyo kuna haja ya kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa Bara. Hii ni mara ya pili kwa Lipumba kutoa kauli hiyo.

Mei mwaka huu, mwenyekiti huyo wa CUF taifa alitoa tamko kama hilo alipoonyesha wasiwasi wake kuhusu upatikanaji wa Katiba Mpya na akasema kwamba, ni hila za CCM za kutaka kumwongezea muda Rais Kikwete. 

Profesa Lipumba ametaja baadhi ya vikwazo ambavyo vinaweza kukwamisha kupatikana kwa Katiba mpya kuwa ni Daftari la Kudumu la Wapigakura kama halijaboreshwa na kasi ndogo ya utoaji wa vitambulisho vya utaifa ambavyo vitatumika kupigia kura hiyo.

Wakati Profesa Lipumba akisema hayo, tayari Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), imeeleza kuwa haina mpango kwa sasa wa kuboresha Daftari la Kudumu Wapigakura kwa ajili ya kura za maoni kwa sababu muda uliobaki ni mfupi.

Kwa mujibu wa radiotehran

0 comments:

Post a Comment