Main Menu

Saturday, November 23, 2013

VUTA NIKUVUTE NA DHAMIRA KUBWA YA UKALE NA USASA NDANI YA KLABU YA SIMBA

Nafasi na wakati wa klabu kama simba, hahahaha kwenye upeo wa hali ya juu mzee wangu Shafi Adam Shafi aliandika kitabu kinachoitwa vuta n'kuvute dhamira kubwa ni ukale na usasa.

Wakoloni walikuwa wanapinga usasa ili waendelee kutawala wakati wazawa walivuta kwenye usasa ili wapate uhuru lakini Shafi adam shafi alimtumia mwanaharakati aitwae Denge kuleta suluhu kwenye jamii ile, simba wanangoja nn? 

Inamaana hakuna watu kama denge? Tatizo la Simba sio Rage na solution sio Kaburu wala Kinesi kwani na wao sio beatiful kwa hili kama alivyosema mwandishi mmoja wa ghana anaitwa aikwey yamah'' kwenye beatiful ones are not yet born, suluhu ya simba ni katiba mpya itakayoifanya klabu ile iendeshwe kibiashara kwa mfumo wa kampuni.

Fikra za baraza la kina mzee hamisi kilomoni haziwezi kwenda na kasi ya maisha ya sasa, ifikie mahala tuondokane na ukale tuliorithi kwa wakoloni tuachane na mabaraza ya wazee tuachane na baraza la wadhamini hayana maana twende kwenye usasa utaoifanya simba ipige hatua.

Simba inahitaji kuwa na rais ambaye anapatikana kwa kumiliki hisa nyingi na si busara za baraza la wazee au wanachama waliohongwa kwenda kumpigia kura jamaa flani.

Simba inahitaji wakurugenzi wataoweza kwenda kasi na changamoto za maisha ya kisasa, mimi sio mshabiki wala mnazi wa vilabu vikubwa vya hapa nchini lakini mimi nimuumini wa maendeleo nimepata fikra kama denge alivyokuwa suluhisho la kuwatoa watawala wa kikoloni walikuwa wanaamini ukale lakini hawakuangalia nafasi ya wakati simba inahitaji mabadiliko ina miaka 77 lakini asset kubwa mpaka leo ni wanachama wahongwaji wanaothaminiwa wakati wa vikao tu.

Majengo mawili ambayo ni posho za kuwalinda wazee wa klabu, timu haina uwanja hata wenye hadhi kama ule unaotumiwa kwenye shule za msingi za tz bado mnasema mnataka flani awe mwenyekiti hamuoni kama mnahitaji mabadiliko mazima ya mfumo mzima wa kiuongozi.

Wacha nikaoge nijiandae na merside derby kwani kule kunawatu wanaojitambua.

NA Issa maeda wa ebony fm

0 comments:

Post a Comment