Main Menu

Saturday, November 16, 2013

SPIKA MAKINDA AWAHUTUBIA MASPIKA MBALIMBALI UMOJA WA MATAIFA, NEW YORK


 Mhe.  Anne Makinda ( Mb),Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano,  akichangia  uzoefu wa  Tanzania katika  ujenzi wa utawala wa kidemokrasia na ushirikishwaji  wananchi na nafasi ya  Bunge na wabunge katika ujenzi wa demokrasia hiyo ni katika mkutano uliokuwa ukijadili mada kuhusu utawala wa kidemokrasia na nafasi yake katika  malengo ya maendeleo endelevu,   Mhe. Spika  alikuwa ni miongoni wa  jopo hilo lilowashirikisha  kutoka kushoto Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  Jan. Eliasson,  Balozi Pauel Seger wa  Usiswi katika Umoja wa Mataifa,  Mhe. Anne Makinda,   Balozi Eduardo Ulibarri wa Costa Rika katika Umoja wa Mataifa, Senator Aitzaz Ahsan kutoka Pakistan, na Ms. Gunilla Carlsson aliyewahi kuwa  mjumbe mashuhuri kuhusu masuala ya ajenda za maendeleo baada ya 2015 na  pia aliwahiki  kuwa  Waziri wa zamani wa  Ushirikiano wa Maendeleo wa Sweden 

 Mhe. Spika akisisitiza jambo katika siku ya pili ya mkutano wa mwaka wa maspika na wabunge kutoka mabunge mbalimbali  duniani wakati walipokutana hapa Umoja wa Mataifa

  Sehemu ya wabunge wakifuatiliana na kushiriki majadiliano hayom,  aliyekaa kwenye kiti  kirefu ni muongoza majadiliano,  Nermeen Shaikh Mtangazani na mtayarishaji wa vipindi kuhusu masuala ya  Demokrasia sasa
  Mhe. Spika akibadilishana mawazo baadhi ya maafisa na wafanyakazi wa Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, wapo pia maafisa kutoka  Wizara za fedha na   Mambo ya nje na   Ushirikiano wa Kimataifa wanaohudhuria mijadala ya   Kamati mbalimbali za Umoja wa Mataifa
Kusikiliza alichosema Mhe. Spika katika mkutano huu BOFYA MSHALE HAPO CHINI


0 comments:

Post a Comment