Main Menu

Wednesday, July 24, 2013

ZITTO KABWE AMPONGEZA MHARIRI MTENDAJI WA MWANANCHI COMMUNICATIONS, BAKARI MACHUMU

Hongera ndugu Bakari Machumu, Mhariri Mtendaji wa Mwananchi Communications

Napenda kuchukua fursa hii nikiwa mmoja wa wasomaji wa magazeti ya Mwananchi na Mwenyekiti wa Kamati ya PAC, kukupongeza kwa kuteuliwa kwako kuwa Mhariri Mtendaji.


Magazeti yenu yameonyesha uhuru mkubwa kwa kuandika habari za ukweli, zilizofanyiwa utafiti na kwa utaalamu wa hali ya juu sana. Natumai chini ya uongozi wako utaendelea kuenzi heshima hiyo ya magazeti ya Mwananchi Communications. 


Changamoto kubwa sana kwa nji yetu ni Ufisadi (rushwa) na Umasikini wa wananchi wetu licha ya kuwa tunaishi kwenye nchi tajiri sana kwa rasilimali na watu pia. Sababu moja kubwa ya kuendelea kwa hali hii ni ukosefu wa UWAJIBIKAJI. 
 
Vyombo vya habari ni silaha kubwa sana ya kuhakikisha utamaduni wa uwajibikaji unaimarishwa nchini kwetu. Hii ni kazi magazeti ya Mwananchi imefanya kwa muda mrefu, lakini haitoshi. 
 
Juhudi lazima ziongezwe kuhakikisha kuwa viongozi wa kisiasa wanajua kuwa matendo na maneno yao kamwe hatapita bila kuhojiwa (Accountability and Answerability for actions and inactions). 


Nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya PAC, ambayo ina majukumu makubwa ya kuimarisha uwajibikaji nchini, Napenda kukutia shime kuhakikisha kuwa magazeti yenu yanashirikiana nasi kupambana na ufisadi na umasikini nchini kwa kuimarisha uwajibikaji. 


Nakutakia kazi njema wewe binafsi na waandishi wote wa Mwananchi Communication. 


Zitto Kabwe
Mwenyekiti PAC
Bunge la Tanzania

0 comments:

Post a Comment