Main Menu

Wednesday, July 24, 2013

RAIS WA SUDAN KUSINI AMEWAFUTA KAZI MAWAZIRI WAKE WOTE.

Rais wa taifa jipya la Sudan Kusini amewafuta kazi mawaziri wake wote. 

Rais Salva Kiir, mwezi uliopita aliwafukuza mawaziri wawili muhimu, na kuanzisha uchunguzi kuhusu madai ya kashfa za ufisadi wa mamilioni ya dola. 


Agizo la rais kuhusu uamuzi wa kulifukuza baraza zima la mawaziri lilisomwa jana jioni kwenye kituo cha televisheni ya taifa. 


Tangazo hilo lilisema kuwa rais Kiir amewaachisha kazi mawaziri wote, pamoja na makamu wake, na ameamuru katibu mkuu wa chama tawala SPLM afanyiwe uchunguzi. 

Sudan Kusini ilijitangaza rasmi kuwa taifa huru mwezi Julai mwaka 2011.

0 comments:

Post a Comment