Main Menu

Monday, July 29, 2013

TIMU YA TAIFA YA MAREKANI YATWAA UBINGWA WA AMERIKA KASKAZINI


Timu ya taifa ya Marekani imetwaa ubingwa wa kombe la mataifa ya Amerika kaskazini baada ya kuifunga timu ya taifa ya Panama kwa goli moja kwa sifuri.


Marekani wametwaa taji hilo maarufu kama kombe la dhahabu kwa mara ya tano na ikiwa ni mara ya kwanza kutwaa ubingwa huo chini ya kocha raia wa mjerumani Jurgen Klinsmann.


Jurden  Klinsmann alishuhudia timu yake ikitwaa taji hilo huku yeye akiwa jukwaani baada ya kufungiwa kwenye mechi ya  nusu fainali dhidi ya Honduras, Marekani walijipatia goli  pekee kupitia kwa mshambuliaji Brek Shea.


Ilikuwa fahari ya aina yake kwa kikosi cha timu ya taifa ya Marekani kutwaa taji hilo ambapo kocha Jurden Klinsman alishuka jukwaani na kushangilia taji hilo akiwa na wachezaji wa akiba kabla hata ya kipyenga cha mwisho hakijapulizwa.

0 comments:

Post a Comment