Inavyoonekana mashabiki wa Rihanna wameanza
kuchoshwa na tabia yake ya uswahili wa kuchelewa kwenye maonesho yake, na
safari hii baadhi walimuandalia dawa yake kwa kuamua kumwagia chips jukwaani
baada ya kuchelewa kufika katika onesho lake la Diamonds huko Manchester,
Uingereza.
Japo akili ya mwimbaji huyo wa Diamonds
haikujiongeza haraka kuutumia ule mwamvuli wake maarufu ‘Umbrella’ kujikinga na
chips hizo kutoka kwa mashabiki hao ambao pamoja na hasira lakini bado
walimngojea kwa hamu.
Rihanna (25) alichelewa kwa saa moja tu, lakini hii
si mara ya kwanza kuchelewa katika matamasha yake na kuwafanya mashabiki
waliofika kwa wingi kumwona wapandwe na gadhabu.
Mwezi (march) mwaka huu alichelewa
masaa 2 katika onesho lake la Montreal, Canada na (July 6) akiwa amelewa
chakali alichelewa tena masaa mawili katika show yake ya Poland.
Mrembo huyo wa Barbados baada ya kupokea zawadi hiyo
(chips) kutoka kwa mashabiki wenye gadhabu akiwa jukwaani alijibu mashambulizi
hayo kwa maneno makali “There’s a good crazy and there’s a bad crazy.
When you
throw s*** up here, that’s an epic fail.
I wanna get your gifts but I don’t want you to knock my people out”.
0 comments:
Post a Comment