Ratiba
ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2013/2014 inayoshirikisha timu
24 zilizo katika makundi matatu zikicheza kwa mikondo miwili (nyumbani
na ugenini) inatarajiwa kutolewa Agosti 14 mwaka huu.
Kundi
A linaundwa na timu za Burkina Moro ya Morogoro, JKT Mlale (Ruvuma),
Kimondo SC (Mbeya), Kurugenzi Mufindi (Iringa), Majimaji (Ruvuma),
Mkamba Rangers (Morogoro), Polisi (Iringa) na Polisi (Morogoro).
African
Lyon (Dar es Salaam), Friends Rangers (Dar es Salaam), Green Warriors
(Dar es Salaam), Ndanda (Mtwara), Polisi (Dar es Salaam), Tessema (Dar
es Salaam), Transit Camp (Dar es Salaam) na Villa Squad (Dar es Salaam)
zinaunda kundi B.
Timu
za kundi C ni JKT Kanembwa (Kigoma), Mwadui (Shinyanga), Pamba
(Mwanza), Polisi (Dodoma), Polisi (Mara), Polisi (Tabora), Stand United
(Shinyanga) na Toto Africans (Mwanza).
Tunapenda
kukumbusha kuwa dirisha la usajili kwa madaraja yote ni moja ambapo
usajili wa hatua ya kwanza ni kuanzia Juni 15 hadi Agosti 3 mwaka huu
wakati hatua ya pili ni Agosti 14 hadi 29 mwaka huu. Dirisha dogo
litafunguliwa Novemba 15 hadi Desemba 15 mwaka huu.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
0 comments:
Post a Comment