Main Menu

Friday, July 26, 2013

JERRY SLAA AZINDUA RASMI KAMBI YA REDDS MISS ILALA

MEYA wa wilaya ya Ilala, Jerry Slaa amewataka warembo wa wilaya ua Ilala kuangalia mbele zaidi mara baada ya shindano hilo waone kuna vitu wamejifunza ili kuweza kuwasaidia katika maisha yao ya baadae.
 
Slaa aliyasema hayo juzi alipowaalika warembo hao katika ofisi zao kwa lengo la kuizundua rasmi kambi ya Miss Ilala katika shindano linalotarajiwa kufanyika Agosti 16 kwenye ukumbi wa Golden jubilee Tower uliopo katikati ya jiji la Dar es Salaam.
 
“Naomba muangalia baada ya mashindano ya Miss Ilala, nini mmenufaika nacho ili kuweza kuwasaida zaidi huko mbele ya safari, lakini vile vile kufanya kazi za kijamii na kuondoa dhana kwamba urembo ni uhuni,” alisema Slaa.
 
Aliwataka warembo hao kuwa wapesi wa kubuni na kujifunza mambo ili nao waweze kuwasaida wenzao lakini pia wao mfano kwa wengine na kuwahamasisha njia mbalimbali za kukabiliana na maisha na kuwajenga moyo wa kutokata tama.
 
Katika mkutano huo ambao warembo walimuuliza maswali mbalimbali Meya huyo kijana mwenye upeo mkubwa wa uongozi, ataungana na warembo hao katika kufanya kazi mbalimbali za kijamii na kujitolea katika wilaya ya Ilala katika kipindi cha mwezi mmoja watakaokuwa kambini.
 
Jumla ya warembo 15  wa Kanda ya Ilala walianza mazoezi rasmi katika ukumbi wa  klabu Billicanas juzi iliyopo katikati ya jiji la Dar es Salaam na Mkurugenzi wa WMP Promotion, William Malecela inayoandaa shindano hilo, alisema jana kanda yake itahusisha warembo kutoka vituo vya Tabata, Ukonga na Mzizima na Dar city centre.
 
Taji hilo kwa sasa linashikiliwa na Noela Michael, mshindi wa pili ni Magdalena Munisi na mshindi wa tatu alikuwa Mary Chizi ambao waliwakilisha kanda ya Ilala katika mashindano ya Miss Tanzania mwaka jana.
Warembo hao watakuwa chini ya mwalimu wao, Suzy Makassy akisaidiwa na Otelia Johnsen kutoka Norway huku Edda Sylvester ni pamoja na  Alice Issac, Clara poul,Maria Peter, Anna Johson, Iren Mwelolo,Rehema Mpanda,Martha Gawe, Diana Joackim, Natasha Mohamed, Dorice Mollel, Pendo Lema, Kazunde Mussa na Kabula Kibogoti
 
 Malecela alisema, pia kutakuwa na jopo la wakufunzi wa dansi, litakaloongozwa na msanii Japhet  aliyekuwa katika kundi la kuibua vipaji la Tanzania House of talent (THT) yote katika kuhakikisha shoo ya mwaka huu inaendana na ubora wa warembo wanaoshiriki shindano hilo.
 
Ilala imewahi kutoa warembo kadhaa miaka ya nyuma, waliopata mafanikio katika mashindano hayo, mitindo na kazi nyingine hasa kupata uzoefu wa kujiamini katika nyanja mbalimbali za urembo na ubunifu wa mavazi.
 
Miongoni mwao ni Hoyce Temu, Jacquliney Ntuyabaliwe, Angela Damas na Salha Israel.
 
Shindano hilo linalotarajiwa kuwa na burudani ya kipekee limedhaminiwa na kinywaji cha Redd’s, Dodoma Wine, magazeti ya Jambo Leo na Tanzania Daima, Blogu ya Wananchi (Le Mutu),  CXC Africa Tours & Safaris, Clouds FM, Times FM, Delina Enterprises.

0 comments:

Post a Comment