Main Menu

Tuesday, June 4, 2013

MAAFISA WA POLISI KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI WAELEKEZWA MATUMIZI YA KIFAA CHA KUPIMIA ULEVI KWA MADEREVA


Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani – DCP. Mohammed R. Mpinga (kulia) na Mkurungezi wa Operesheni Upturn Group Co - Mr. Muhata Denis (kushoto) wakijadiliana jambo kuhusu kifaa cha kupimia ulevi (alcohol test) wakati wa semina ya Siku mbili ya kipima ulevi (alcohol test) yaliyohusisha maafisa na askari wawakilishi wa Kikosi cha Usalama Barabarani kutoka baadhi ya mikoa Tanzania bara.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani – DCP. Mohammed R. Mpinga (katikati) akipewa taarifa fupi kuhusu semina ya siku mbili ya kifaa cha kisasa cha kupima ulevi madereva kutoka kwa Mkurungezi wa Operesheni wa kampuni ya (Upturn) - Mr. Muhata Denis (kushoto kwa Kamanda).
Picha inayoonyesha kifaa cha kipimia ulevi madereva (alchol tester) wakati wa semina ya siku mbili ya kujifunza kifaa hicho iliyofanyika katika Chuo cha Polisi Dar es salaam
Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani kutoka baadhi ya mikoa Tanzania bara ambao ni washiriki wa semina ya siku mbili ya kifaa cha kupimia ulevi (alcohol tester) wakifanya mazoezi ya namna ya kutumia kifaa hicho.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani – DCP. Mohammed R. Mpinga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja iliyohusisha maafisa na askari wawakilishi wa semina wa Kikosi cha Usalama Barabarani kutoka baadhi ya mikoa Tanzania bara. Semina hiyo ilifanyika katika Chuo cha Polisi Dar es salaam - Kilwa road tarehe 29/05/2013 – 30/05/2013.


0 comments:

Post a Comment