Main Menu

Monday, April 22, 2013

MAANDAMANO KUPINGA SHERIA YA NDOA YA JINSIA MOJA YAENDELEA NCHINI UFARANSA

Kumekuwa na maandamano ya dakika za mwisho mwisho mjini Paris, siku mbili kabla ya bunge la Ufaransa kuidhinisha sheria inayohalalisha ndoa za jinsia moja. 


Wanaopinga sheria hiyo walikusanyika katika eneo la Montparnasse la mji mkuu katika juhudi za mwisho mwisho za kuizuia sheria hiyo. 


Maandamano mengine ya kundi hasimu pia yaliandaliwa jana kuiunga mkono sheria hiyo. 


Zaidi ya watu 100 wamekamatwa katika kipindi cha wiki moja iliyopita katika maandamano mengine ya kupinga ndoa za jinsia moja. 


Makundi ya kutetea haki za binadamu pia yameripoti ongezeko la matusi na mashambulizi ya kimwili dhidi ya jamii ya mashoga na wasagaji nchini Ufaransa. 

Ufaransa inatarajiwa kuwa nchi ya 14 kuhalalisha ndoa za jinsia moja, kufuatia kuidhinishwa sheria hiyo nchini New Zealand wiki iliyopita.

0 comments:

Post a Comment