Barua zilizokuwa zimetumwa kwa Rais
Obama na Seneta wa Mississippi,
zilizobainika kuwa na sumu hatari aina ya
ricin zinahusiana. Idara kuu ya upelelezi ya
Marekani FBI imetoa taarifa hiyo.
Barua hizo zote zilitumwa kutokea Memphis,
Tennessee.
Mtu mmoja mwenye umri wa miaka 45
amekamatwa Mississippi kuhusiana na barua
hizo.
Pamoja na barua hizo, polisi mjini
Washington wanavichunguza vifurushi vitatu
vya mashaka vilivyogunduliwa katika ofisi za
majengo ya seneti.
Kugunduliwa kwa vifurushi hivyo kwenye
eneo kubwa la majengo ya serikali
kumesababisha wasiwasi,na idara za
usalama zimeongeza ulinzi.
Barua kwa Rais Obama na Seneta Wicker
zilitumwa tarehe 8 kabla ya mashambulio ya
mabomu mjini Boston.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment