Main Menu

Friday, May 29, 2015

SEPP BLATTER ASHINDA UCHAGUZI WA FIFA, JE ENGLAND, UEFA ZITATEKELEZA ILIYOAHIDI...?



Victory: Sepp Blatter (pictured) celebrates after his re-election as president of FIFA in Zurich on Friday nightHatimae Joseph Sepp Blatter amefanikiwa kutetea kiti chake cha urais wa shirikisho la Soka Duniani FIFA baada ya kumuangusha mpinzani wake mwana wa Mfalme Ali Bin Al Husein.

Katika uchaguzi huo uliofanyika katika jiji la Zurich Uswiss blatter amepata kura 133 dhidi ya 73 za mpinzani wake katika Round ya kwanza.

Kutokana na matokeo hayo upigaji kura ulitakiwa urudiwe lakini Prince Ali akajitoa na kumpa nafasi Blatter kutangazwa mshindi.
 Blatter beat Prince Ali bin al-Hussein by a margin of 133-73 in the first round of voting, forcing his withdrawal
Kwa matokeo hayo Blatter mwenye umri wa miaka 79 ataongoza kwa miaka 4 akikabiliwa na changamoto ya tuhuma za rushwa zinazowakabili maofisa wa taasisi hiyo, uchunguzi unaoendeshwa na mamlaka za marekani.

Lakini pia atakabiliwa na tishio la UEFA la kugomea michezo ya kufuzu kwa kombe la dunia la mwaka 2018, tishio lililotolewa na rais wa UEFA Michel Platini siku ya alhamisi.
Disappointment: Following the win, the Chairman of the England Football Association Greg Dyke (right) said FIFA 'will not reform itself under Blatter'
Naye mwenyekiti wa fa ya England Greg Dyke aliiambia Sky News kuwa England itajiondoa katika michuano ya FIFA kama Blatter ataendelea kuongoza.

Kwa madai kuwa hakuna mabadiliko yoyote yanayoweza kutokea chini ya Blatter ambaye ameshakaa madarakani kwa miaka 16.

Katika hotuba yake baada ya ushindi Blatter amemshukuru na kumpongeza mpinzani wake kwa kusema alikua mshindano wa kweli.

Kuhusu sakata la rushwa linaloshikiliwa kidete na Marekani na Uingezeza, Blatter amesema kama mataifa hayo yangepata nafasi ya kuandaa kombe la dunia hayo yote yasingetokea.Blatter is all smiles as voting gets underway at the FIFA Congress. The voting phase took 90 minutes

0 comments:

Post a Comment