Klabu ya Chelsea imesema kuwa kipa wake
namba mbili msimu huu Petr Cech yupo huru kuongea na klabu yoyote inayotaka
kumsajili.
Cech alijiunga na klabu ya Chelsea mwaka 2004 akitokea
klabu ya Rennes ya nchini Ufaransa na kufanikiwa kuchukua mataji mengi akiwa na
Chelsea.
Ujio wa kipa aliyekuwa kwa mkopo katika klabu ya Atletico
Madrid Thibaut Courtois kunako klabu ya Chelsea, umemlazimu kocha wa Chelsea
Jose Mourinho kumtumia Cech kama kipa namba mbili.
Wakala wa Petr Cech Viktor Kolar amesema mteja wake
anawaniwa na vilabu vingi vikiwepo vilabu vya Arsenal, Inter Milan, Besiktas na
Liverpool.
Katika maisha yake kunako klabu ya Chelsea, Petr Cech
amefanikiwa kuchukua makombe ya Ligi Kuu ya soka nchini England, Kombe la FA, Ligi
ya Mabingwa Ulaya na Europa League.
0 comments:
Post a Comment