Main Menu

Wednesday, August 20, 2014

ROJO AELEKEA MANCHESTER KUKAMILISHA DILI LAKE LA UHAMISHO.

KLABU ya Manchester United imekubali kutoa Pauni Milioni 16 kumnunua beki wa Sporting Lisbon, Marcos Rojo.
 
Rojo, ambaye ametua mjini Manchester leo na kusema kuhamia United ‘anahisi kama ndoto’, anatarajiwa kusaini Mkataba wa miaka minne akifaulu vipimo vya afya na kukubali vipengele binafsi vya mkataba wake.
 
Winga Luis Nani, aliyejiunga na United kutoka Sporting kwa Pauni Milioni 17 mwaka 2007, amerejeshwa kwa mkopo klabu yake hiyo ya zamani, ikiwa ni sehemu ya dili hilo la Rojo.
Marcos Rojo akiwasili England leo kwa ajili ya kukamilisha usajili wake Manchester United

0 comments:

Post a Comment