Main Menu

Wednesday, July 17, 2013

SNOWDEN AOMBA HIFADHI YA MUDA URUSI, PUTIN AAHIDI KUMPA

Mfanyakazi wa zamani katika shirika la upelelezi la Marekani Edward Snowden ameomba hifadhi ya muda nchini Urusi, ambako amekuwa akiishi kwa wiki tatu zilizopita. 


Idara ya uhamiaji ya Urusi ilithibitisha jana kuwa imepokea maombi ya raia huyo wa Marekani, ambaye amekwama katika uwanja wa ndege wa Moscow. 


Hayo yameripotiwa siku chache baada ya Snowden kukutana na wanaharakati wa haki za binadamu, na kutangaza nia yake ya kuomba hifadhi ya muda nchini Urusi, kabla ya kuhamia katika nchi za Amerika Kusini zilizompatia hifadhi ya ukimbizi. 


Marekani imekwishaifuta pasipoti ya Snowden, na inafanya kila juhudi kumkamata na kumfungulia mashitaka ya ujasusi, baada ya kufichua mpango wa nchi hiyo kuchunguza mawasiliano ya watu binafsi na nchi washirika. 


Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema Urusi itampa hifadhi Snowden, ikiwa ataacha mienendo inayoweza kuharibu uhusiano wa Urusi na Marekani.

0 comments:

Post a Comment