Main Menu

Monday, July 29, 2013

KAMISHNA JENERALI WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI AWAVISHA VYEO MAAFISA WAKE, JIJINI DAR ES SALAAM LEO



Naibu Kamishna wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Luteni Kanali Lidwino Saimon Mgumba (kushoto) akimvisha cheo Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Iringa, Mrakibu Msaidizi wa jeshi hilo, Kennedy Komba katika hafla fupi iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Zimamoto na Uokoaji, jijini Dar es Salaam leo. Naibu Kamishna Mgumba aliwavisha vyeo maafisa hao kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, Pius Makuru Nyambacha. 
Naibu Kamishna wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Luteni Kanali Lidwino Saimon Mgumba akiwaasa maafisa wa jeshi hilo waliovishwa vyeo katika Ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Zimamoto na Uokoaji jijini Dar es Salaam leo. Mgumba aliwaasa maafisa hao kutumia vyema vyeo na madaraka waliyopewa kwa uhadilifu na kwa kuzingatia sheria. Naibu Kamishna Mgumba aliwavisha vyeo maafisa hao kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, Pius Makuru Nyambacha. 
Baadhi ya Maafisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji pamoja na askari wakimsikiliza kwa makini Naibu Kamishna wa jeshi hilo, Luteni Kanali Lidwino Saimon Mgumba wakati alipokuwa akiwaasa maafisa wa jeshi hilo waliovishwa vyeo katika Ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Zimamoto na Uokoaji jijini Dar es Salaam leo. Mgumba aliwaasa maafisa hao kutumia vyema vyeo na madaraka waliyopewa kwa uhadilifu na kwa kuzingatia sheria. Naibu Kamishna Mgumba aliwavisha vyeo maafisa hao kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, Pius Makuru Nyambacha. 


Picha zote na Puyo Nzalayaimisi, Afisa Mahusiano wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Makao Makuu.


0 comments:

Post a Comment