Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Symbion Power Tanzania Limited zimesaini
makubaliano ambapo kampuni hiyo itasaidia kwenye maeneo matatu ya mpira wa
miguu wa vijana.
Makubaliano
hayo yametiwa saini leo (Februari 26 mwaka huu) kwenye ofisi za TFF jijini Dar
es Salaam. Rais wa TFF, Jamal Malinzi amesaini kwa niaba ya shirikisho wakati
upande wa Symbion aliyesaini ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Peter Gathercoles.
Maeneo
ambayo Symbion itasaidia ni ujenzi wa vituo viwili vya kuendeleza vipaji
vitakavyojengwa Kidongo Chekundu na Kinondoni mkoani Dar es Salaam, mashindano
ya Taifa ya wachezaji wenye umri wa chini ya miaka 12 (U12) yatakayofanyika
mwaka huu na kuisaidia timu ya U17 ya Tanzania (Serengeti Boys).
Serengeti
Boys itacheza na Afrika Kusini, Julai mwaka huu katika mechi za mchujo kuwania
tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa wachezaji wa umri huo zitakazofanyika
mwakani nchini Niger.
Hivyo
Symbion imetoa dola 60,000 (zaidi ya sh. milioni 96) kwa ajili ya mashindano ya
U12, na dola 50,000 (zaidi ya sh. milioni 80) kwa ajili ya maandalizi ya
Serengeti Boys kwa mechi dhidi ya Afrika Kusini.
Rais
Malinzi ameishukuru Symbion kwa kukubali kushirikiana na TFF katika mpira wa
miguu wa vijana, lakini vilevile amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Jakaya Kikwete kwani ndiye chachu ya kampuni hiyo kuamua
kujishirikisha na mpira wa miguu wa vijana.
ZAMBIA WATUA
KUIKABILI TWIGA STARS
Timu
ya Taifa ya Zambia (Shepolopolo) inatua nchini kesho mchana (Februari 27 mwaka
huu) kwa ajili ya mechi ya marudiano ya michuano ya Afrika kwa Wanawake (AWC)
dhidi ya Tanzania (Twiga Stars) itakayochezwa keshokutwa (Februari 28 mwaka
huu).
Shepolopolo
yenye msafara wa watu 29 itawasili kwa ndege ya Fastjet ikitokea Lusaka na
itafikia kwenye hoteli ya Accomondia kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa
Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi kuanzia saa 10 kamili jioni.
Waamuzi
wa mechi hiyo kutoka Burundi wakiongozwa na Ines Niyosaba wamewasili nchini leo
asubuhi wakati Kamishna Fran Hilton-Smith kutoka Afrika Kusini atawasili kesho
(Februari 27 mwaka huu) saa 8 kamili mchana kwa ndege ya South African Airways.
Boniface Wambura Mgoyo
Media and Communications Officer
Tanzania Football Federation (TFF)
0 comments:
Post a Comment