Main Menu

Thursday, April 16, 2015

KUISHUHUDIA YANGA VS ETOILE DU SAHEL BUKU TANO



Klabu ya soka ya Yanga imetangaza viingilio vya mchezo wake dhidi ya Etoile du Sahel utakaofanyika siku ya jumamosi katika uwanja wa taifa Dar  es salaam.

Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa klabu hiyo Jerry Murro amesema kiingilio cha chini katika mchezo huo kitakua shilingi 5,000.

Kiingilio cha juu ni shilingi 40,000 ambapo itakua VIP A, VIP B shilingi 30,000, VIP C shilingi 20,000 na jukwaa rangi ya chungwa shilingi 10,000.

Murro amesema tiketi za mchezo huo zitaanza kuuzwa kesho katika vituo mbalimbali jijini Dar  es salaam.

Baadhi ya vituo hivyo ni uwanja wa Karume, Ubungo stand, Dar live Mbagala, Mwembe Yanga, Buguruni sheli, Feri kivukoni, Bilicanas na makao makuu ya klabu ya Yanga.

0 comments:

Post a Comment