Main Menu

Friday, April 10, 2015

KOCHA WA STAND UNITED AFUNGUA MILANGO KWA TIMU NYINGINE



Kocha Emanuel Masawe (katikati) akizungumza na wachezaji wake katika chumba cha kubadilishia nguo.

Kocha wa timu ya Stand United aliyesimamishwa na uongozi wa timu hiyo Emanuel Masawe amesema milango ipo wazi kwa timu yoyote inayohitaji huduma yake.

Masawe ambaye hivi karibuni aliripotiwa kutua kuifundisha timu ya Polisi Moro amesema tangu uongozi wa Stand United ulipotangaza kumsimamisha haujampa barua yoyote ya kusimama kwake.

Amesema yeye bado ni kocha wa timu hiyo ambayo aliipandisha ligi kuu kutoka ligi daraja la tatu hadi pale mkataba wake utakapo malizika mwezi wa saba.

Katika kusisitiza hilo amesema hata alivyokwenda kufanya mazungumzo na uongozi wa timu ya Polisi Moro aliwataarifu viongozi wa Stand ambao kimsingi bado ana mkataba nao.

Hata hivyo Masawe amesema mazungumzo yake na uongozi wa Polisi Moro hayakufikia muafaka na hivyo kushindwa kufanya nao kazi huku akiahidiwa kuitwa msimu ujao kama itafanikiwa kubaki ligi kuu.

Masawe ambaye ana leseni Class B ya caf anasema hivi sasa yupo tayari kufanya kazi  na klabu yoyote sehemu yoyote barani Afrika ambapo leseni yake inamruhusu.

Emanuel Masawe ambaye anamkubali zaidi kocha Sunday kayuni wa Tanzania na Jose Mourihno wa Chelsea japo hapendi style ya uchezaji wake ni kaka wa mchezaji wa Ndanda Fc Jacob Masawe.

0 comments:

Post a Comment