Mchezaji Amissi Tambwe aliwasilisha malalamiko dhidi ya
Simba ya kutolipwa dola 7,000 za Marekani zilizotokana na klabu hiyo kuvunja
mkataba wake Desemba 15, 2014.
Uamuzi wa kuvunja mkataba ulikuwa ni wa makubaliano
ya pande zote ambapo Simba ilitakiwa iwe imemlipa fedha hizo mlalamikaji
kufikia Desemba 17, 2014.
Katibu Mkuu wa Simba SC , Steven Ally alikiri klabu yake
kudaiwa na mchezaji huyo na kuwa wameshafanya mawasiliano na wakili wake
aliyepo Ureno, Felix Majani na kupanga utaratibu wa kulipa isipokuwa
kinachosubiriwa ni kusaini hati ya makubaliano ya malipo (Deed of Settlement).
Kamati imesikitishwa na klabu ya Simba kushindwa kumlipa
mchezaji huyo kama ilivyokuwa katika makubaliano ya kuvunja mkataba
yaliyofikiwa na pande zote mbili Desemba 15, 2014.
Klabu ya Simba inatakiwa kumlipa Amissi
Tambwe fedha hizo kwa awamu mbili. Awamu ya kwanza ya dola 5,000 malipo yawe
yamefanyika kufikia Aprili 30, 2015. Salio la dola 2,000 ili kukamilisha jumla
ya dola 7,000 liwe limelipwa kufikia Mei 10, 2015, uamuzi ambao upande wa Simba
ulikubaliana nao.
0 comments:
Post a Comment